WANACHAMA WA KLABU YA MAJIMAJI WAJITOLEA ZOEZI LA UKARABATI WA UWANJA WA MAJIMAJI
Na Andrew
Mhaiki, Mwanaperamiho blog
WANACHAMA wa
klabu ya Majimaji ya Songea, tawi la Amshawasha
lililopo Msamala mjini hapa wamejitokeza kufanyakazi za
kujitolea katika kusaidia ukarabati wa uwanja wa Majimaji
katika kazi za kusambaza kifusi cha mchanga na
kupanda nyasi(ukoka) ikiwa ni sehemu ya kuwaunga mkono
wadau wa soka katika harakati zao za kuhakikisha uwanja
huo unaotumika kucheza ligi ya Vodacom msimu ujao
Akizungumza mjini hapa jana Mwenyekiti wa tawi hilo la Amshawasha, Salehe
Shaweji alisema kuwa wanachama wa klabu ya Majimaji tawi la
Amshawasha wamekuwa wakitekeleza kauli mbiu ya mkoa ya "Ruvuma
kwanza" ikiwa na lengo la kuhakikisha Ruvuma inarejea
kwenye ramani ya soka kama ilivyo kwa miaka nyuma,
Alisema tawi hilo limeungana na wadau wengine wa soka katika kazi ya
ukarabati wa uwanja huo wa Majimaji baada ya kubaini wamiliki wa uwanja
huo ambao ni chama cha Mapinduzi(CCM) kususia kufanyakazi hiyo kwa kisingizio
cha ukosefu wa fedha wakati ligi ya Vodacom inakaribia kuanza Majimaji
ikiwa miongoni mwa vilabu ambavyo vitakavyoshiriki ligi hiyo hapa
nchini.
Alisema baada ya kubaini hilo wanachama wa tawi hilo kwa
umoja wao waliamua kuhamasishana na kwenda kufanya kazi hiyo ya
kusambaza kifusi cha mchanga pamoja na kupanda ukoka ikiwa moja wa
mchango wao kwa klabu hiyo ya Majimaji huku akidai pamoja na zawadi kwa
Wanaruvuma ambao wamekuwa na kiu kubwa ya kuhakikisha timu yao ya
Majimaji inatumia uwanja huo kwenye mechi zake za nyumba kucheza
ligi hiyo,
Mwenyekiti huyo pia alisema pamoja na kuiona Majimaji ikicheza kwenye
uwanja huo bado kwa wafanyabiashara watakuwa na fursa nzuri za kiuchumi kwa
kujiongezea kipato cha kifedha wakiwemo wafanyabiashara wa nyumba
za wageni, mamalishe na wenye vyombo vya usafiri kutokana na kuwepo kwa wageni
watakao kuja kuishuhudia Majimaji ikicheza nyumbani kitu
ambacho kimekuwa kikililiwa kwa mikoa ambayo haina timu inayoshiriki ligi kuu
ya Tanzania Bara.
Naye
mlezi wa tawi hilo la Amshawasha, Joseph Nswila alipohojiwa na mwandishi
wa habari hizi wakati wakiendelea na hilo zoezi la kusambaza kifusi na
kupanda ukoka alisema tawi hilo lenye wanachama 60 limekuwa likifanyakazi
ya kujitolea pamoja na kuchangia fedha kwa ajili ya Maendeleo
ya klabu yao ya Majimaji, huku likifanya kazi ya kuhamasisha wakazi wa
mkoa wa Ruvuma ndani na nje ya mkoa wahakikishe Ruvuma inakuwa
kimaendeleo kupitia soka kwa kutumia kauli ya mkoa ya " Ruvuma
kwanza"
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni