Alhamisi, 9 Julai 2015


CHAMA KISICHOTAMBULIKA KISHERIA CHAENDESHA LIGI YA SOKA HUKO MPITIMBI NA KUWAACHA WAKAZI WA KATA HIYO WAKIBAKI BABAIKONI

Na   Andrew   Mhaiki, wa Mwanaperamiho blog.

BAADHI  ya wadau wa soka  kutoka vijiji vya  kata ya  Mpitimbi  huko Songea  vijijini  wamelalamika   kuwa viongozi  wao wa Serikali  ya kata hiyo  wamekuwa  wakiendesha  mashindano  ya soka kinyume  cha sheria  kwa  madai  kuwa wao  wanafuata   miongozo, taratibu, sheria  na kanuni  za   chama cha  soka  Tanzania (FAT) ambayo  imepitwa  na wakati   badala ya   ya  Shirikisho la mpira  wa miguu  Tanzania(TFF)

Walisema  pamoja  na viongozi  wao wa Serikali  ya kata hiyo  kudai  wanafuata   miongozo, taratibu, sheria  na kanuni  ambazo zilizowekwa  na  chama chao cha  FAT, bado  kata hiyo ya Mpitimbi  kwa upande  wa soka inasimamiwa  na chama cha soka cha Songea vijijini (SORUFA)  ambacho  kipo  kisheria  na  kimesajiliwa  kupitia msajili wa vyama vya michezo na vilabu nchini na  kina mamlaka  ya kusimamia   mashindano  yote  ambayo yanayoanzishwa  vijijini  na si  vinginevyo. 

Walisema  viongozi  hao  ambao  wanadai   chama  chao cha FAT  kipo kisheria  na kimesajiliwa  kupitia  kwa msajili  wa vyama vya  michezo  na vilabu  nchini na  kina mamlaka  ya kusimamia  na  kuendesha  mashindano  ya soka  bila  ya  kupitia  kwenye  uongozi  wa SORUFA ,  kwa kutumia uongozi  wao .

Mmoja  wa wadau  hao wa soka, Lezley  Francis  mkazi  wa kijiji  cha  Mpitimbi “B'  katika  kata hiyo  alipohojiwa  na Mwanaperamiho blog  alisema  hatua  iliyofikia  ya viongozi  wa  Serikali  ya kata hiyo  ya kuunda  chama  chao  cha FAT na  kuendesha  na kusimamia  mashindano  mbalimbali  imekuwa ikiwashangaza  baadhi  ya wadau  wa soka, kwani  alidai SORUFA  ndio  chama pekee  ambacho  kipo  kisheria  na si  hicho  chama  chao  ambacho  wanachodai  kipo  kisheria  kupitia  msajili  wa vyama vya michezo  na vilabu  nchini.

Alisema  kama  taasisi au vyombo  husika  hawataliona  hilo  na kupiga  marufuku  kwa kuwachukulia  hatua  za  kisheria  viongozi  wa chama  hicho  cha FAT ambacho  wanadai  kipo kisheria, kuna uwezekano  mkubwa  wa kutokea  kwa mgogoro  kati  ya FAT  na SORUFA  kwani  kila chama  kinaweza  kuja na madai  kuwa wao ndio  wenye mamlaka   ya  kusimamia  na kuendesha  soka  katika wilaya hiyo na kupelekea   kuviyumbisha  vilabu  wakati  vikijiandaa na mashindano  ya  ligi ya Daraja  la Nne  msimu huu.

Naye  Katibu Mkuu wa  FAT, John  Njovu  alipohojiwa na blog hii  juzi  kijijini  hapo  alisema  chama chake  kipo  kisheria  na kina uongozi  kamili na  kina katiba  yake  na kimekwisha kamilisha  usajili kupitia kwa usajili  wa vyama vya  michezo  na vilabu nchini,  huku akidai wana haki  ya kusimamia  na kuendesha  mashindano  ya soka  kwa mujibu  wa katiba  yao.

Kwa upande  wake,  Katibu  Mkuu wa SORUFA, Idefonce  Luoga  alipohojiwa  juu ya chama  hicho  kipya  cha FAT  ambacho  kipo katika wilaya hiyo, alisema  kwa misingi na taratibu na kanuni  za Shirikisho  la soka  nchini (TFF) ambapo  watekelezaji  wake  kwa ngazi  ya mkoa  chama cha soka cha mkoa  wa Ruvuma(FARU) na  kwenye  wilaya hiyo  ya Songea vijijini kinatambulika chama kimoja  ambacho  SORUFA  ndio  wenye  majukumu  ya kikatiba  ya  kusimamia  na kuendesha   mashindano  yote  ya soka katika wilaya hiyo  na si vinginevyo.

Hata  hivyo  Ofisa  michezo  wa  halmashauri hiyo ya Songea  vijijini, Ndingo  Zamngoni  alipohojiwa  na gazeti hili  jana  ofisini  kwake  juu ya kuwepo kwa chama kipya cha soka katika wilaya yake  ambacho  kimesajiliwa kwa  jina la FAT  alidai  hana  taarifa  anachokitambua  ni SORUFA huku akisema  kuwa kwa mujibu  wa sheria  kwa  ngazi  ya  mkoa   chama  kimoja na wilaya kunakuwa na chama kimoja na si  viwili na wanachama  wao  vilabu  vya  soka  vilivyosajiliwa  na visivyosajiliwa , huku  akiahidi  kufuatilia  na kuona  usajili  wao ambapo  alidai kwenye  orodha  ya vyama vilivyokuwa na usajili  chama hicho  cha  FAT  hakipo  katika wilaya hiyo.

Huku, Katibu  Mkuu wa chama cha  soka mkoa wa Ruvuma(FARU), Ahmed  Challe  alipohojiwa  juu ya kuwepo  kwa chama kipya cha soka  ambacho  kimesajiliwa  kwa jina la FAT ambacho  kimeanza  kazi ya  kuendesha  na kusimamia  mashindano  katika vijiji vya   halmashauri ya wilaya ya Songea   alisema  FARU  kwa mujibu  wa taratibu, sheria  na kanuni  za soka ambayo  iliyoundwa  na Shirikisho  la soka  Duniani(FIFA) na kutekelezwa  na Shirikisho  la  soka nchini(TFF)  na  imeshuka  na kutumika  kwenye  ngazi ya  vyama   soka  vya  mkoa  na wilaya  alidai  kwa kuepuka  migogoro  na vurugu  viongozi  wa chama  hicho wanatakiwa wakamatwe  na wafikishwe  Mahakamani  kwa kosa la kunyakua  madaraka  kinyume  cha  sheria za soka.

 Chama  hicho  kipya  cha FAT  kwa sasa  kinaendesha na kusimamia  mashindano  ambayo  yanayoshirikisha  vilabu  vitano  kutoka vijiji vya kata  hiyo ya Mpitimbi, huku Songea vijiji ikiwemo Tonosa  Fc, Mseo  Fc, Mkurumusi  Fc, Stendi  Fc na Muungano Fc  ambapo ada  ya ushiriki  Sh 15,000  kwa  kila  kilabu na inaendeshwa  kwa mtindo  wa ligi  ya mzunguko   mmoja , huku   timu  ambayo  itakayokiuka  taratibu, sheria  na kanuni  itatozwa  faini ya Sh 20,000
MWISHO



         
Makamu Mwenyekiti wa Chama halali cha mchezo wa Soka, Wilaya ya Songea Vijijini (SORUFA) Bw. Hamdani Hamdani.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni